Lyrics Labs
Mapenzi Basi Lyrics - Artist : Diamond Platnumz
Mi mwenzenu tena basi
Oh mapenzi sitaki
Oh mwenzenu tena basi
Basi sitaki
[x2]

Yalinifanya nikaugua
Mara napanga napangua
Mwili ukakonda nikapungua
Ah sikulala, sikulala
Oh maradhi nikaugua oh
Yakanichoma na kuungua roho
Kutwa nawaza na kuwazua
Sikulala

Hayo mapenzi bwana, hayana maana
Yalinifanya mi nichekwe
Sababu yake nshagombana, nikatukanwa
Lakini akanipiga teke
Ai haya mapenzi bwana, hayana maana
Yalinifanya mi nichekwe
Sababu yake nkagombana, usiku mchana
Yeye

Mi mwenzenu tena basi
Oh mapenzi sitaki
Oh mwenzenu tena basi
Basi sitaki
[x2]

Oh nilishagombana na mama mzazi
Akataka nimwagia radhi
Sababu yule fulani, yule wa moyo wangu
Yakaleta zengwe kwa kazi
Ugomvi wa simba na panzi
Vurugu kwa majirani
Ah, ee Mola wangu

Hayo mapenzi bwana, hayana maana
Yalinifanya mi nichekwe
Sababu yake nshagombana, nikatukanwa
Lakini akanipiga teke
Ai haya mapenzi bwana, hayana maana
Yalinifanya mi nichekwe
Sababu yake nkagombana, usiku mchana
Yeye

Mi mwenzenu tena basi
Oh mapenzi sitaki
Oh mwenzenu tena basi
Basi sitaki
[x2]

Copyright © 2009-2024
Privacy policy - DMCA Policy - Contact Us